Uaminifu kwa kanuni zilizofunuliwa katika neno la Mungu  na kuzingatiwa katika asili

Kudumisha  Mashamba na Jamii

Tunafundisha mbinu za ukulima ambazo zinalenga  kilimo hai, kilimo endelevu na ambazo zimeendelezwa Afrika kupitia Misingi ya Ukulima Tunazisaidia jamii kuanzisha mashamba madogo ya mboga za jikoni, kuwaonyesha kutengeneza mbolea, kuhimiza na kuwa na jitihada  katika kilimo ambacho kinaweza kuleta faida.

Kila kitu tunachokifanya lazima kifanywe  kwa wakati, kwa kiwango cha juu, bila uharibifu na kwa furaha. Kwa kanuni hizi, wakulima wadogo wanaweza kufurahia fadhila ya dunia.

"Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza" Mwanzo 2:15
Wakulima wa Mashambani

Tunaamini kuwa wakulima wa mashambani katika vijiji kote ulimwenguni wanaweza kuwa na maisha tele kwa kujifunza kutunza ardhi vizuri kwa njia inayostahili. Tunafanya kazi kuwafundisha  mbinu bora zaidi za ukulima.

Wenye njaa wa Ulimwengu

Asilimia 98 ya wenye njaa duniani wanaishi katika nchi zinazoendelea.
Asilimia 75 kati yao wanaishi vijijini, hasa katika vijiji vya Asia na Afrika, na
Asilimia 70 kati yao wanategemea kilimo kama kazi yao.

Ndiyo sababu tumejitolea kuwafikia, kuandaa na kuwatia moyo.

Kupambana na udumavu

Angalau watoto milioni mia moja hamsini na sita (156,000,000) ulimwenguni kote wamedumaa na athari za maisha mabaya ya afya na  matatizo ya mapato. Walio chini ya lishe bora huchangia zaidi ya thuluthi moja ya vifo vyote. Kwa kuwafundisha ukulima wa kifamilia tunatafuta kupambana na udumavu wa watoto katika ulimwengu wote.

Mipango yetu ya ukulima

Hapo chini kuna baadhi ya miradi tunayoendeleza kwa sasa na njia unazoweza kuhusika.

Mradi huu |
Inaendelea
Inaishia
Mashamba madogo ya familia 
Ili kuwezesha familia za mashambani kuwa na kujitegemea na kutoa fursa kwa biashara, tunasambaza mbegu za kuanzia na vifaa vinavyohitajika kuanzisha ukulima wa mashamba madogo. Wanafanya mengine yaliyo salia kwa msaada wa wakufunzi wetu wa FARM STEW!
Mradi huu |
Inaendelea
Inaishia
Mafunzo
Wakufunzi wetu wa FARM STEW wanasisitiza kanuni za kila mojawapo ya viungo vyetu vinane katika madarasa tunayoyafunza. Shughuli za kiutendaji hufanya masomo  kuchangamsha na kuwasaidia washiriki kustawi!