Kutoa fursa ya kuwezesha kupata chakula endelevu na mapato

Kufanya biashara ndogondogo kuwezekane

Tunaamini kwamba Mungu anatamani  watu wote wawe na maisha tele kwa hivyo  tunazingatia kazi yetu ya ujasiriamali kwa  biashara ambazo zitasababisha afya na ustawi. Kilimo chenyewe ni biashara ambayo lazima ianzishwe na akili yenye mtazamo wa kupata faida ili iwe endelevu. Madarasa yetu ya upishi kwa njia ya utendaji hutoa ujuzi wa kuanza viwanda vya kinyumbani.

"Lakini twawasihi ndugu mzidi sana.Tena mjitahidi kutulia na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe." 1 Thess. 4:10-12
Biashara ndogondogo

Ujuzi mwingi tunaofundisha husababisha uwezo wa kutengeneza bidhaa (k.m ukulima, kupika). Wenyeji wamezingatia maarifa mapya na kuanzisha biashara zao ndogondogo za kuuza bidhaa mpya wanazozitengeneza nyumbani.
Familia nyingi zimeanzisha biashara endelevu za kutengeneza mandazi  ya soya na maziwa ya soya.Tunawahimiza na kuwandaa kwa ajili ya mafanikio

Kukabiliana na ukosefu wa usawa

Kwa elimu tunayowafunza, fursa mpya za biashara zinapatikana kwa wanaume na wanawake vijana na wazee. Hasa katika tamaduni ambazo wanawake hawana  njia ya kujipatia fedha, mabadiliko madogo yanaweza kuleta tofauti nzuri. 

Uendelevu

Badala ya vitini, FARM STEW inaamini katika biashara. Ndiyo sababu tunauza mbegu, kwa kiwango cha kupunguzwa sana, kwa wakulima wa mwenyeji.

Katika siku za usoni, makampuni ya Vyakula ya FARM STEW barani Afrika yataanza kuzalisha vyakula vinavyopatikana nchini kwa rejareja, huku asilimia 100 ya faida itatengwa kuendeleza kazi ya FARM STEW ya kufikia jamii.


Miradi yetu ya biashara

Hapo chini kuna baadhi ya miradi tunayoendeleza kwa sasa na njia unazoweza kuhusika.

Mradi huu |
Inaendelea
Inaishia
Mafunzo
Wakufunzi wetu wa FARM STEW wanasisitiza kanuni za kila mojawapo ya viungo vyetu vinane katika madarasa tunayoyafunza. Shughuli za kiutendaji hufanya masomo  kuchangamsha na kuwasaidia washiriki kustawi!