Ilichapishwa
Oktoba 1, 2019

Kuchelewa mno kwa Jovia

Joy Kauffman, MPH

Jennifer, mamake Jovia, alikumbatia ujumbe wa FARM STEW. Mkufunzi wetu, Dan Bautama (katika kijani) alianza kufanya kazi katika jamii yake ya vijijini Mashariki mwa Uganda miezi michache iliyopita. Kwanza alilenga sana juu ya "usafi" wakati alitambua kwamba kulikuwa na vyoo vichache sana na hakukuwa na vituo vya kuosha mikono. Watoto wenye kutokwa na kamasi puani wanahakikisha jambo hili.

Shukrani kwa msaada wako, wakati Joy alipowasili mwezi Mei, mabomba ya mifereji yalikuwa kila mahali na jamii ilifanya maendeleo mengi. Walikuwa na furaha kushiriki yote waliyokuwa wamejifunza!

Jennifer alipenda  bomba lake la mfereji sana kwamba nilimuonyesha akinawa mikono katika ukurasa wetu mpya wa  Masomo ya kimtandao ya kujifunza nyumbani. Niliangalia picha hii mara nyingi wakati huu wa majira ya joto kama tunavyojiandaa kwa bidii kwamba siku moja itabariki mamilioni (tunatumaini) na kichocheo cha FARM STEW cha maisha tele.

Jennifer anaosha mikono yake kwenye bomba lake jipya la tippy, na Dan (katika kijani) na jamii ikishiriki wakati huo. Jovia anapumzika mgongoni mwa Jennifer.

 Nililia mwezi uliopita nilipopokea habari hii kutoka kwa Dan:

"Habari Bi. Joy , kwa huzuni kubwa natangaza kifo cha mtoto wetu mpendwa  kutoka kikundi cha FARM STEW cha Buwambiidhi. Natumai unakumbuka  mtoto huyo wakati  tulipotembelea kijiji hicho katika mashamba ya miwa. Tulikuwa tumekuja kwa mafunzo leo, kwa bahati mbaya, tulikumbana na habari za huzuni, sasa tunahudhuria mazishi. "

Mbona ninatoa machozi hata sasa?

Kitakwimu, Jovia ni mmoja wa mamilioni, lakini kifo chake kilikuwa cha kipekee kwa familia yetu ya FARM STEW na kwangu. Baada ya miezi michache ya mafunzo ya FARM STEW katika jamii ya Buwambiidhi Mashariki mwa Uganda, bustani ndogo za  jikoni zilikuwa zimeanza kuzalisha chakula. Wanakijiji walilima kwa bidii maeneo yazungukayo nyumba zao.

Joanita, mkufunzi wa FARM STEW, hufanya kazi na wanakijiji pamoja na Jovia katika kijiji cha Buwambiidhi wakiwa katika bustani zao mpya ya FARM STEW.

Cha kusikitisha, kama unavyoona hapo juu, mengi ya yale tuliyofundisha kuhusu "ukulima,"ingawa hayakuweza kutekelezwa ni kwa sababu shamba linalozunguka kijiji  lilikuwa limetengewa upanzi wa miwa badala ya vyakula vya virutubishi vingi. Mikataba ya miaka mingi  kutoka makampuni ya kimataifa huleta majaribu kwa watu maskini lakini  huishia kupata hasara zaidi kuliko faida.

Hiyo ndiyo sababu mafunzo yetu ya "Ujasiriamali" ni muhimu sana!

Nilipokutana na Jennifer, mara moja nilikuwa na wasiwasi na nywele za mtoto wake Jovia. Sehemu nyekundu za viraka vya nywele zilizokunjana zilibaini mtoto aliyekuwa na utapiamlo sana. Nilimwambia Dan atusaidie kuzungumzia jambo hili. Baada ya kujifunza kwamba Jennifer alikuwa akimlisha Jovia uji wa mahindi sana, nilidhani Jovia alikuwa akikosa protini, madini ya chuma, vitamini  C ambayo ingesaidia kunyonya madini ya chuma na pia vitamini B.

Jennifer alisita  kiasi kwa sababu hakuweza kufikiria kwamba mtoto wake mdogo  mnene Jovia angeweza kuwa na utapiamlo. " Si ukubwa wake unaashiria malezi yangu mazuri kama mama?" alionekana kushangaa.

Tulipendekeza kwamba Jovia alihitaji kwenda katika  uchunguzi wa kimatibabu.Tulimpa Jennifer ushauri  wa  kunyonyesha kama inavyohitajika na kuanza kumlisha Jovia aina mbalimbali za vyakula  vya kupikwa na kupondwa vinavyopatikana kienyeji. Dan alirudi muda mfupi baadaye  na kuanza upanzi wa miche ya mboga. Alilenga sana juu ya lishe, mafunzo ya  "chakula" chetu.

Lakini Jovia alikuwa amechelewa sana. Jovia alipata malaria na kufariki kwa sababu ya upungufu wa damu ambao ni ukosefu wa  madini ya chuma.

Biblia inasema kwamba "Uhai wa mwili uko katika  damu" (Mambo ya Walawi 17:13) na ni kweli. Bila ya madini ya chuma, chembechembe zako nyekundu za damu haziwezi kutoa oksijeni kwa mwili wako na chembechembe zako kwa kweli hukosa hewa. Hivyo ndivyo ilitokea  kwa Jovia.

FARM STEW imeundwa ili kushughulikia ukweli unaovunja moyo kwamba  katika Afrika ya Kusini mwa jangwa la Sahara, watoto 5 wenye umri wa chini ya miaka 5 hufa kila dakika. Wengi  hawana majina na vifo vyao havitagusa maisha yetu lakini Jovia ni tofauti. Tunafahamu kisa chake na jina lake.

Ndiyo maana tumeweka wakfu  Masomo yetu ya mtandao ya kozi ya  FARM STEW kwa kumbukumbu yake.

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Joy Kauffman, MPH
Joy ni mwanzilishi mwenye shauku wa FARM STEW.
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.