Ilichapishwa
13 Julai, 2018

Matokeo mabaya ya sukari

Joy Kauffman, MPH

Sukari,katika hali yake safi nyeupe na fuwele huonekana bila madhara lakini sisi sote tunakubaliana kwamba ikiwa nyingi inaweza kusababisha mianya kwenye meno na kuongeza uzito zaidi. Hata hivyo, meno yetu huitamani na mahitaji yake ulimwenguni hayajawahi kupanda. Hata hivyo, katika njia ambazo huenda usiifikirie, ina madhara makubwa kwa watoto.

Je umewahi kuona ukikua?  Muwa hukua wima na kwa urefu.  Ni aina ya mti  wa kudumu unaostawi katika hali ya hewa ya kitropiki, zao la kuuzwa, linalokuzwa na makampuni mengi ya kimataifa katika nchi maskini.  Katika hali ya  kejeli mbaya,    miwa ni sehemu ya kisa kinachosababisha  milioni 58,000,000 ya  watoto wa kiafrika  kuwa na  ufupi wa uliokithiri na matokeo mabaya yasioweza kugeuzwa

Je, watoto wafupi wanahusikanaje na miwa? Je, wote wanaweza kuchangiaje umaskini? Ili kujua, ninawaalika kuja katikakijiji cha Wagona, mashariki mwa Uganda.

Paa la umaskini na vibanda vya matope vilivyotawanyika  katika njia nyembamba zilizofunikwa na kivuli cha mashina ya miwa. Wakati makampuni makubwa yalipohama  muongo mmoja uliopita, wanakijiji wengi waliacha kukuza mazao yenye virutubishi vingi kama vile mtama  na kunde kwenye mashamba yao madogo.  Wanakijiji walibadili chakula kwa ajili ya ahadi ya fedha. 

Robert, mtaalamu wa kilimo wa Farm Stew Uganda , anaarifu  kwamba "familia nyingi zinakosa chakula  kwa sababu nchi yote inatumika kwa ajili ya kukuza  miwa ya sukari badala ya kukuza chakula. Watoto hupatwa na magonjwa ya lishe na afya mbaya ya familia kwa ujumla. "

 Kwa muda, thamani ya miwa imepungua kwa kiasi kikubwa kwenye soko la wenyeji.  "Mazao ya kuuzwa" yanaweza kuwaacha familia kuwa na umaskini uliokithiri!  Ni mzunguko mbaya na watoto wanakabiliwa vibaya zaidi ya yote.

 Nashukuru, kupitia  zawadi zako,FARM STEW inatoa suluhisho!

FARM STEW  iliendesha mafunzo yake ya kwanza huko Wagona na washiriki 55, tarehe 23 Januari 2018.  Mafunzo  ya ziada ya  vikao vya kiutendaji ya siku mbili   yalifanyika katika wiki zilizofuata, ambapo watu 88 walishiriki kikamilifu.  Kwa kufundisha viungo vinane vya kichocheo cha maisha tele vya FARM STEW (Ukulima, Mtazamo, Mapumziko, Chakula, Pumziko, Usafi,  Ujasiriamali, Maji)tunaziandaa familia hizi kuvunja mzunguko wa umaskini, kuwahimiza kurudi kwa maadili ya chakula cha kinyumbani na kiwanda cha kienyeji.

Mwezi uliopita, Robert, (mwenye mavazi ya kijani), alitumia wakati na wakazi wa Wagona, David na mkewe Fatuma wakati wa moja ya ziara nyingi za nyumbani za FARM STEW  katika jamii. Robert alivutiwa sana na bustani yao mpya iliyostawi.  David, Fatuma na familia nyingine nyingi, walionyesha matokeo ya mbinu walizojifunza kutoka kwa FARM STEW.

Kwa furaha, Fatuma alisema, "Kabla ya kuja kwenu, fedha kidogo mume wangu alizopata kama mshona viatu  hazikutosha kulisha familia na kulipa karo za shule kwa ajili ya watoto wetu wanane.   Niliogopa kulima (kilimo) kwani nilifikiri ilikuwa ni laana. "

Hisia hiyo ya huzuni ni ya kawaida tu. Watu wengi wanaamini kuwa bustani ya mboga ni zaidi ya uwezo wao na chini ya heshima yao. Kwa  $15 tu kwa kila familia $150) kwa 10, tunaweza kushinda kikwazo na kuwasaidia kuanza bustani.

FARM STEW inawakumbusha wanakijiji  ukweli rahisi wa kibiblia kwamba tuliumbwa katika bustani na kuambiwa tuitunza. (Mwanzo 2:8, 15) wakati huo, hakukuwa na laana na Mungu alitangaza kila kitu kilikuwa "kizuri sana!" 

Kupitia kwa usaidizi wako wa ukarimu, tunaweza kuwafikia watu ambao ni miongoni mwa maskini na wenye njaa zaidi duniani.  Tunawakumbusha kwamba watu wa Mungu walikuwa ni wakimbizi na maskini sana. Mungu alituma ujumbe kupitia nabii Yeremia (29:5) kwa watu wake akisema, ""Jengeni nyumba, mkakae ndani yake, kapandeni bustani, mkale matunda yake."

David na Fatuma walijifunza kwa dhati!  Alielezea, "baada ya FARFM STEW kutufundisha manufaa ya bustani na kutupa mbegu za mboga, ilinibadilisha maisha yangu.  Sasa ninajiona kama mtu muhimu sana katika jamii yangu. Kwa kupanda mboga, tuna uwezo wa kuziandaa na kula na zimetuboredha afya yetu. Baadhi ya watu katika jamii sasa huja kununua mboga. Sasa nina mboga katika hatua zote za ukuaji; katika kitalu, na zile ambazo zimekua na zilizo tayari kuvunwa. Kwa kuuza za ziada, sasa ninaweza kupeleka watoto wangu shule na kuangalia mahitaji ya msingi ya nyumbani, hivyo kumsaidia mume wangu."

  

Robert akiwa na Fatuma na David wakivutiwa na biringana zao.  David anashughulikia  bustani yake ya nyumbani aliyoitayarisha akiwa miguu chuma 

Wanandoa hawa wenye furaha, wananikumbusha juu ya ukweli rahisi ambao FARM STEW inazingatia, "wakati mbinu sahihi za kilimo zinapotumika,  umasikini utapungua sana kuliko ulivyo sasa. Tunakusudia kuwapa watu mafunzo ya utendaji  juu ya kuimarika kwa nchi, na hivyo kusababisha kulima ardhi yao, ambayo haitumiki kwa sasa.

 Tukikamilisha hili, tutakuwa tumefanya kazi nzuri ya utume. " (EGW, barua 42, 1895)

Hongera kwa kazi yako nzuri, lakini kisha pumua  kwa kina kwa kuwa kuna kazi nyingi za kufanywa bado.  Turudie watoto wafupi, sukari na umaskini, Je, wana kitu gani sawiya wote? Kwa neno moja tu, utapiamlo.

Watoto hawa wa kiafrika wenye umri wa miaka 9 wanaweza  wasionekane kuwa watapiamlo.  Unaweza kufikiria  ni wafupi. Nani anayejali? Lakini ni  wakati  gani ufupi ulikuwa kitu kibaya

Watoto hawa wa kiafrika wenye umri wa miaka 9 wote wamedumaa ikilinganishwa na kiwango cha urefu cha shirika la afya ulimwenguni.

Jibu ni, kudumaa, hufafanuliwa kama urefu kwa umri ulio  chini ya kawaida. Huwezi tu kuangalia watoto na kujua kama wamedumaa  lakini bado ni aina  ya utapiamlo iliyo mbaya zaidi .

 

Kama aina nyingine za utapiamlo, madhara ya kudumaa hayabadiliki.   Athari zake hujumlisha ukosefu wa uwezo wa kujifunza,  ukosefu mbaya wa mafanikio, hatimaye upungufu wa uzalishaji, afya mbaya na unene kupita kiasi.

 

Ndio maana kuzuia ni muhimu na kwa nini  Farm Stew  inalenga familia na ujumbe wa ukamilifu. Sababu za kudumaa ni lishe duni na maambukizi yanayojirudia hasa katika siku 1,000 za kwanza za maisha.  Muda mfupi, kutoka utunzi wa mimba hadi miaka miwili, huamua mustakabali wao.

Je, hiyo inahusianaje na sukari?   inanishawishi pamoja na timu zetu.

Nilipokuwa nchini Uganda miezi michache iliyopita, mimi na Julius, mmoja wa wakufunzi wa FARM STEW, tulikuwa tukitembea kupitia maeneo ya miwa  kuelekea kijiji ambacho tulikuwa tunafanya mawasiliano ya kwanza. Njiani tulimkuta kijana huyu mdogo aliyekuwa akilia akiwa amekaa chini ya tonobari la plastiki na kitu kidogo cheupe katika mkono wake. 

Tulijua jina lake, Yusufu, na kwamba mama yake alikuwa amefariki. Wakati baba yake alikuwa akifanya kazi katika mashamba ya sukari, 

Aliachwa siku nzima na kitita cha miwa atafune. Nilivunjika moyo, lakini baadaye katika maombi, alinitia nguvu kupitia aya hii. 

"Tena tusichoke katika kutenda mema, maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho."  Wagalatia 6:9 

HafarijikiSiku nilipokutana na Joseph akiwa ameshikilia miwa mkononi!

Watoto wengi kama Joseph wanateseka kutokana na njaa, magonjwa na umaskini.  Hawapati kile ambacho miili yao michanga inachohitaji ili ikue.   Shauku ya FARM STEW ni kuwafikia.  Uchaguzi wako wa kufanya vyema, kupitia  zawadi yako, inaruhusu timu zetukutokufa moyo!

Mimi nimebarikiwa sana kwamba umechagua kufanya uwezekano wa kuwafikia watu 34,295 na mafunzo yetu hadi sasa.  Wito unakuja kutoka vijiji vingi.  Tuna mtumaini Mungu, lakini ni juu yenu  kufanya iwezekane.

Kichocheo cha maisha tele, kimejengwa juu ya msingi wa sayansi ya kuthibitika, miongo ya utafiti katika maendeleo ya kimataifa na Biblia. Matokeo yake ni kwamba maisha  yanabadilishwa kimwili, kiakili na kiroho.  Je unaweza kusaidia kupanua na kuimarisha tuwafikie watu zaidi?

Nina uhakika kuwa maisha ya Joseph bado ni magumu lakini majuma machache baada ya tukio hili, timu yetu ya FARM STEW iliweza kurudi katika kijiji chake kuwapa mafunzo wenyeji kuhusu vyakula vya virutubishi vidogo ambavyo wanaweza kumudu kuvitengeneza na kuwapa watoto kama yeye.  Tukiongozwa na Yesu, masomo yetu huhimiza wenyeji kuwa na huruma kwa wadogo kati ya hawa  kama Joseph.  

 

Nimetiwa moyo sana na visa vya familia za Uganda ambazo zinawafikia watoto kama Joseph. Kwa mfano, huko Jinja, Uganda tumekuwa na mafunzo katika makao ya nyumba za  mayatima zinazosimamiwa na wenyeji. Ni watu waliosadiki mwito wao wa kujali 

  Mwanamke mmoja kwa jina la   Samara ana watoto 60 wenye matatizo ya kukua katika nyumba yake.  Anashangazwa na walivyo bora kwa chakula  kipya cha bei nafuu na mabadiliko rahisi katika usafi na mtazamo.  Yeye pamoja na  asilimia themanini (80%) ya wale wote waliofanyiwa utafiti wanaipa heko Farm Stew kwa kazi nzuri yenye athari muhimu katika maisha yao. 

Je, utaendelea kushirikiana na watu kama vile Samara  ili kufikia watoto kabla  wadumae

Je, utawezesha familia au kijiji chote kujifunza kichocheo cha maisha tele?  Ninawauliza na kuwaomba kufikiria zawadi ya kusaidia  FARM STEW

 Naweza kuwahakikishia kuwa, pamoja na wanakijiji, mtavuna mavuno tele.  

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Joy Kauffman, MPH
Joy ni mwanzilishi mwenye shauku wa FARM STEW.
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.