Ilichapishwa
12 Julai, 2019

Wakimbizi wapambana na dhana potovu za hedhi 

Joseph Malish

Makala hii ilionekana katika New Vision, Gazeti linaloongoza la Uganda

Margaret Dipio wa miaka 43 aliondoka Sudani Kusini mwaka 2014 na aliwekwa katika makazi ya wakimbizi ya Boroli katika wilaya ya Adjumani kaskazini mwa Uganda.  Kwa kuishi miongoni mwa watu wenye asili tofauti ya utamaduni, hivi karibuni, Dipio alitambua mitazamo mbalimbali ya kikabila kuhusu hedhi. Moja ya mitazamo ambayo amekumbana nayo  ni kwamba kipindi cha hedhi ni hali iliyona kasoro kibaolojia, kwa hivyo msichana hutengwa  kila mwezi anapopata hedhi. Msichana hatarajiwi kugusa chombo chochote cha kupikia licha ya kumsalimia mtu yeyote.

 

Kwa ujumla, yeye huonekana kuwa mchafu na mbaya zaidi ya wote hasa kama hedhi zake zinakuja na maumivu, huhusishwa na laana ya mababu. Katika makazi ya Boroli, baadhi ya tamaduni huaminika kwamba msichana katika kipindi chake lazima huwa na shimo sawa na ukubwa wa sehemu yake ya nyuma, ambayo hutarajiwa kukaa kwa masiku bila kuoga mpaka hedhi yake iishe.

 

Imani hizo hapo juu zaonyesha kwamba hakuna mtu anayepaswa kuigusa damu ya hedhi inayotoka hasa isije ikasababisha huyo msichana kuwa tasa baadaye. Kwa hiyo, mikakati mikali imewekwa ili kuzuia hili kutokea. Hicho ni kiwango cha hadithi za kizamani za jadi juu ya hedhi ambazo Dipio na wengine wachache wako nje ili kukabiliana kati ya chuki kali kutoka sehemu ya Kihafidhina ya jamii yake.

 

Wakiwa na tumaini dogo la mafanikio, Dipio na wengine walianza kuzungumza na viongozi wenye ushawishi na wa kidini kuhusu hitaji la msururu huu wa mawazo finyu kuhusu  hedhi. Kikundi hicho kilitembelea shule na makanisa ili kuzungumzia usafi wa hedhi pamoja na kusisitiza haja ya jamii kuacha mila ambazo zinawarudisha nyuma wanawake katika makazi ya wakimbizi wa Boroli na ulimwenguni kote

 

"Baadhi ya wanawake wanaogopa kuwaambia waume zao kuhusu kuwanunulia visodo  wasichana wao," Dipio alisema.

 

Margaret, akiwa nyumbani kwake, anapenda kuhudumu na FARM STEW kama mkufunzi.

[Dipio ni mkufunzi wa FARM STEW Uganda, Shirika la Taifa lisilo la kiserikali pamoja na huduma ya kuboresha afya na ustawi wa familia maskini na watu walio katika mazingira magumu.]

 

"Wakati tunapokuja pamoja kukuza mboga, pia tunazungumzia kuhusu shida za wanawake katika jamii yetu," Dipio alisema. Wanatembelea shule za msingi katika eneo hilo kulenga wasichana hasa watano hadi saba kuzungumza nao kuhusu usafi wa hedhi.

 

Dipio pia anatoa mafunzo kwa wasichana kuhusu matumizi sahihi ya visodo. Anasema kuwa ujumbe wao unaingia taratibu katika kujaza upungufu unaoletwa na vikwazo vya utamaduni katika jamii "Wengi wanaacha tabia hiyo mbaya polepole," alisema.

 

Hata hivyo, vita vyao dhidi ya ubaguzi unaohusiana na hedhi,  vinazuiwa na umaskini wa nyumbani katika makazi ya wakimbizi.

 

"Baadhi ya familia haziwezi kujimudu kununua visodo kwa ajili ya binti zao," Dipio alisema.

 

Katika shule ya msingi ya Boroli, mwalimu mkuu wa kike, Harriet Walea, alisema wasichana, hasa kutoka katika makazi ya muda huwa na uwezekano wa kukosa masomo wakati wanapoishiwa na visodo wanavyopewa na mashirika. Sio wazazi wote wanaoweza kununua visodo, kwa hivyo "ni wazi kuwa huacha masomo wakati wa kipindi cha hedhi,"  Walea alisema.

 

Boroli iliandikisha wasichana zaidi ya 497 mwanzoni mwa 2019, Walea anasema idadi imeshuka katika kipindi cha pili. Karibu nusu ya wasichana hukosa madarasa kila siku, wale ambao hukosa wako katika madarasa ya juu. "Tunashuku kwamba hukosa kuhudhuria kwa  sababu ya hedhi zao," Walea alisema.

 

AFRIpads, kampuni ambayo hutengeneza visodo vinavyoweza kutumika tena, imetoa msaada wa 200 [pakiti] ya visodo kwa FARM STEW kusambaza katika shule ya msingi ya Boroli katika kampeni iliyopewa mada ya "hedhi zangu, sauti yangu".

 

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Joseph Malish
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.