Ilichapishwa
Novemba 25, 2019

Kisa cha Phionah

Phionah Bogere

Mimi ni Phionah Bogere mwanamke mwenye furaha wa umri wa miaka 23.

Nilimpoteza mama yangu nilipokuwa na umri wa miezi kumi tu. Baba yangu alifariki nilipokuwa na miaka sita. Kama yatima, nilianza kuishi na dada yangu mkubwa. Nilikuwa nikiamka asubuhi na mapema kwenda kuchota maji katika ziwa la Kyoga ambako kulikuwa mbali sana.

Maisha yalikuwa  magumu. Dada yangu alikuwa na familia yake mwenyewe ya kuitunza   kwa hivyo nilipelekwa katika kituo cha watoto yatima. Kwa namna fulani, kwa njia ya kujitahidi , Mungu aliniruhusu kupata mafunzo  kupitia shule ya ufundi.

Kisha mwaka wa 2015, nilihudhuria mojawapo ya  mafunzo ambayo Joy Kauffman alifundisha katika kanisa langu.

Wakati wa mafunzo, nilikuwa na hamu sana ya kujifunza na nilimuuliza maswali mengi. Wakati ulipoisha, nilimuuliza kama ningeweza kuwa mmoja wa timu yake. Baadaye, nilijifunza kwamba Mungu alikuwa amemwonyesha kuwa anapaswa kuanza timu  ya FARM STEW lakini  bado hakuwa amemwambia yeyote. Swali langu lilikuwa ni uthibitisho tu wa Roho Mtakatifu ambaye alihitaji kufuata usadikikaji wake. Nilikuwa na furaha sana na kushangaa kupata habari kwamba nilikuwa nimechaguliwa kuwa kwenye timu ya awali ya  FARM STEW. Tangu wakati huo nimejifunza mengi.

Mimi binafsi nimefanya mafunzo  243 katika vijiji, shule, hospitali na makanisa na kuwafunza watu 16,694. Tuna karatasi za kuonyesha mahudhurio ya darasa la kila siku   ili kuthibitisha hilo! Ninapenda kutoa mafunzo kwa wanakijiji jinsi ya kukuza na kutengeneza vyakula vipya, vya afya na kuwaelimisha vijana wadogo wa kiume jinsi usafi ulivyo muhimu katika kutunza miili yao.

Hata nami nina bustani la chombo katika nyumba yangu.

Hiyo hunisaidia kuhifadhi mshahara wangu, kuniruhusu kulipa karo za shule kwa ajili ya mayatima.

Kupitia  kwa mafunzo, nimejifunza kujieleza na kupata ujasiri. Pia nimeweza kuhubiri ujumbe wa  Mungu kupitia FARM STEW kwa sababu tunatumia  Biblia kama msingi wa mafundisho yetu.

Ninawashukuru wafadhili wa FARM STEW!

Kwa sababu yenu, washiriki wengi wameboresha afya na tabia za kula na sasa wanafanya kilimo. Ninakutana na watu wengi ambao maisha yao yamebadilishwa kwa kutekeleza kile tunachofunza. Natamani ungekutana nao!

 FARM  STEW iishi maisha marefu! Phionah

Hapa kuna zaidi ya kisa cha Phionah ! Hapa kuna ushuhuda wa dakika 2 wa Phionah! Hapa kuna ushuhuda wa dakika  2 wa Phionah!

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Phionah Bogere
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.