Ilichapishwa
15 Julai, 2020

Kahn katika Zimbabwe na FARM STEW

Kahn Ellmers

Kutana na Kahn, mwanagenzi wa FARM STEW na watoto nchini Zimbabwe katika nyumba ya mayatima ya Newstart!

Nchini Zimbabwe, FARM STEW ya kimataifa ina furaha kushirikiana na Kuda Vana!


Kuda Vana (ambayo ina maana ya "Kupenda watoto" katika lugha ya Shona) ni nyumba ya mayatima ambayo inafanya kazi ya kuwawezesha watoto walio katika mazingira magumu ya Zimbabwe si tu kwa kuishi lakini kustawi. 


Susan Cherne, mwenyekiti wa Bodi ya Kimataifa ya FARM STEW aliwasiliana na  Kuda Vana wakati alipokuwa akihudhuria kongamano la ASI la Kimataifa la mwaka wa 2019  huko Louisville, Kentucky kutafuta njia ambazo mashirika haya mawili yanaweza kushirikiana. Kuda Vana alijifunza kwamba FARM STEW ilikuwa ikifanya kazi ya kuboresha afya na ustawi wa familia maskini na watu walio katika mazingira magumu kwa kushiriki  kichocheo cha maisha tele kote ulimwenguni.Ushirikiano wa asili ulianza na ndoto za kijana mmoja kwa ajili ya siku za usoni yenye kujitoshelezazenye  yalichochewa. 


Kuda Vana si nyumba yako ya mayatima wa kawaida. Wafanyakazi wao hutoa utunzaji wa kimsingi kwa kila yatima au mtoto aliyetelekezwa na kuletwa kwao na huduma za jamii. Watoto wanalelewa katika mazingira ya kinyumbani ya kikundi na kupewa upendo, lishe, usalama, huduma za afya, elimu, ujuzi wa maisha,  mwongozo wa kiroho na kihisia ili kuwawezesha kuishi kwa kujitegemea zaidi, maisha yenye heshima na yaliyo bora. Wakati watoto wanapofikia umri wa miaka 18 katika utunzwaji, mpango wa mpito wa vijana wa Kuda Vana hutoa msaada wa mpito wa makaazi na karo  kwa shule ya biashara au chuo kikuu. 


Kila mtoto katika huduma ya Kuda Vana huchukuliwa kama wa familia na inapowezekana, kusaidiwa katika matumaini yao binafsi na ndoto zao. Hii ndio maaana Kuda Vana alikuwa na wasiwasi kuhusu mustakabali wa kijana Tendai  mwenye umri wa miaka 16 ambaye amekuwa katika nyumba ya  mayatima tangu alipokuwa mtoto. Tendai  ana ulemavu wa kujifunza na kama kijana mdogo mara nyingi alionewa na walimu. Akiwa na umri wa miaka 15, hakuweza kusoma wala kuandika jina lake na alikata tamaa kabisa  kufikia ndoto yake ya kuwa mtaalamu wa kilimo au kujitegemea. 

'

Kwa wakati na huduma kutoka kwa wafanyakazi huko Kuda Vana, Tendai hivi karibuni alijifunza kusoma. Yeye ni kijana wa ajabu ambaye ni mzuri katika kuimarisha mambo na kuchunga bustani huko Kuda Vana. Anaweza kufanya jambo lolote kukuza na huona fahari kubwa katika kazi yake. Hata hivyo, wafanyakazi walikuwa na wasiwasi juu ya kitakachotokea kwa Tendai wakati atakapofika miaka 18 na kuhitajika  kuondoka kisheria katika Chuo cha Kuda Vana. 


Dkt. Rick Westermeyer, Mkurugenzi wa wa kujitolea  FARM STEW ya Zimbabwe, na mke wake alitembelea nyumba ya watoto wa Kuda Vana mwisshoni mwa mwaka. Walitembea katika bustani na kujifunza kuhusu maono ya Kuda Vana ya kuzindua mpango wa Mpango wa kilimo kustawi, mpango wa kuimarisha usalama wa chakula wa shirika na kukuza ujuzi wa maisha muhimu. Miezi michache tu baada ya mpango huu ilizinduliwa, Kuda Vana alikuwa na uwezo wa kuongeza ardhi yao ya kilimo na asilimia 500! 


Dkt. Rick na mkewe pia walijifunza kuhusu Tendai na uhusiano wake na kilimo pamoja na mapambano yake katika shule ya jadi. FARM STEW ya Zimbabwe na African Orhan Care  walijitolea kumpa Tendai udhamini kwa ajili ya kuhudhuria msingi wa mafunzo ya kilimo huko Harare pamoja na mfanyakazi wa FARM STEW wa kujitolea. Nafasi hii ilionekana kuwa kichocheo kamili cha Tendai kwa ajili ya kujiamini  kwa matarajio yake ya baadaye kama mtaalamu wa kilimo. 


Baada ya wiki mbili za kujifunza kuhusu kutengeneza mbolea, matandazo na kutengeneza mazao ya juu kutoka kwenye vipande vidogo vya ardhi, Tendai alipata cheti katika misingi ya kilimo. Kama mwanafunzi mdogo huko, anasema alihisi kukubaliwa na kujumuishwa na kila mtu hasa Khan Ellmers, mfanyakazi wa kujitolea wa FARM STEW   alikuwa  mvumilivu na mwenye manufaa katika kuhakikisha kwamba alielewa kila wazo. Tendai anasema kuhusu uzoefu wake: 


"Ningependa kutoa shukrani zangu na kutoa shukrani kwa watu ambao walinifadhili kuwa na fursa ya kuhudhuria mafunzo haya ya kubadilisha maisha. Siku zote nimekuwa na ndoto za kupata nafasi ya kuwa na mafunzo hayo kwa kuimarisha ujuzi wangu kwani nina shauku kubwa katika kilimo. Sasa nina kitu ambacho naweza kufanya wakati umri wangu utanitoa nje ya Kuda Vana. Ningependa kuwa mkulima mkubwa wmenye uwezo wa kusambaza chakula kwa waduka makubwa ya mboga. Kwa sasa, ninatunza Ustawe wa  mpango wa kilimo wa Kuda Vana, na si kubahatisha: Sasa nafanya mambo sahihi ninapo fanya kilimo. Hiki cheti kinamaanisha mengi kwangu. Hakuna anayeweza kuchukua maarifa niliyo nayo, nami nitachunguza ulimwengu. Kwa mara nyingine tena, asanteni sana kwa msaada. "


FARM STEW ina shukrani kwa ushirikiano wetu na Kuda Vana na ina tarajia  kushirikiana katika njia zaidi ya kuhakikisha watoto walio katika hatari zaidi ya Zimbabwe si tu kwa kuishi bali kustawi. 


Ikiwa ungependa kujifunza zaidi kuhusu kazi ya Kuda Vana na watoto yatima nchini Zimbabwe, tafadhali tembelea www.kudavana.org!

Ili kuona mahojiano kamili na Kahn Ellima bonyeza hapa!

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Kahn Ellmers
Kahn ni baraka kwa FARM STEW kwa wakati huu nchini Zimbabwe!
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.