Ilichapishwa
5 Februari, 2020

Ubunifu wa Umwagiliaji maji wa Jonah

Joy Kauffman, MPH

Tazama uvumbuzi wa umwagiliaji wa Yona kwa vitendo!

Jonah Woira ni mmoja wa wakufunzi wetu bora nchini Uganda. Yeye ana shauku ya kukuza vyakula vya kienyeji, chakula endelevu na kwa ajili ya watu wanaoendelea! Yeye ni mjuzi sana kwa mambo ya kilimo (mtaalam katika sayansi ya usimamizi wa udongo na uzalishaji wa mazao) na tumefurahi kuwa naye kama kiongozi wa maswala ya kilimo wa FARM STEW ya Uganda tangu Oktoba ya 2019.

Mojawapo ya njia ambazo Jonah ameonyesha ujuzi wake ni katika uvumbuzi na ubunifu wake. Katika kijiji cha Kalungami katika wilaya ya Jinja Mashariki mwa Uganda hakuna pampu ya maji. Ile waliokuwa nayo ilivunjika miaka miwili iliyopita. Kwa sababu hakuna mtu aliyewahi kufunzwa jinsi ya kudumisha au kurekebisha pampu wakati kumetokea tatizo. Watu wa kijiji hiki sasa wanalazimika kutembea maili 2 (kama kilomita tano hivi) kupata maji kila siku.

 

Hata hivyo, hii haijasimamisha wanachama wa shule ya nyanjani ya Jonah ya FARM STEW kutokana na kutia bidii katika kumwagilia miche yao ya mboga. Suluhisho la ubunifu wa Jonah lilikuwa kuwafunza mbinu za unyunyiziaji mdogo wa maji kwa kutumia chupa za plastiki zilizotupwa kwa kuziweka juu chini! Hii huokoa safari za  kwenda kuchota na husaidia kuifanya miche yao kuwa na maji na afya.

 

Je, yote haya ni rahisi? Kwa hakika sivyo. Je, mwishowe kuna thamani yoyote? Wale wanaofanya kazi na Jonah wanatoa hakikisho la ndio! Wamechangamshwa na mimea pamoja na mazao yao! Sio tu kwamba wanaweza kulisha familia zao wenyewe bali wanaweza pia kupata fedha kupitia kuuza mazao ya ziada kwa jamii ya eneo hilo.

 

Moja ya vipaumbele 5 vya FARM STEW kwa mwaka wa 2020 ni kurekebisha pampu ya maji katika kijiji cha Kalungami pamoja na kutengeneza visima 19 vingine na kuchimba visima 30 vipya. Ingawa lengo hili litagharimu $150,000, hili litatusaidia  kubariki zaidi ya watu 15,000i! Hatuwezi kusubiri kuona njia za ajabu ambazo Mungu atazitumia kutusaidia kufikia lengo hili!!!

Jonah ameleta na anaendelea kuleta tofauti kubwa katika maisha ya wale anaowafundisha.Tunashukuru sana kwamba yeye ni sehemu ya wafanyakazi waFARM STEW!

"Imekuwa ni hali ya kusisimua ingawa ya changamoto ya uzoefu wa mafunzo kwangu. Imefungua akili na moyo wangu kwa uwezo ambao watu wanao na kwa utayari wao wa kujifunza, kufanya mazoezi na kusaidia jamii zao. Wenyeji wengi sasa wanatumia ujuzi mpya wa kilimo. Wengi wa watu hawa walikuwa hawajawahi kutaka kusikia kuhusu injili, hata hivyo sasa  wanaulizia masomo ya Biblia! Wanaona kwamba tuna furaha sana kufundisha kila mtu na kutoa wakati wetu na rasilimali, inawasisimua. Mtazamo wetu wa unyenyekevu na utayari wa kusaidia si jambo la kawaida unaloweza kuliona hapa,"Yona Woira alisema.

Jonah Woira na baadhi ya wanawake kutoka kijiji cha Kalungami

Je, unapenda jinsi mbinu kamili yaFARM STEW ya kuendeleza watu inashughulikia sababu za msingi za njaa, magonjwa, na umaskini? Bofya kitufe cha zambarau nzuri upande wa kulia wa ukurasa ili kusaidia kuweka miradi kama vile ya Yona  kwa nguvu!

Asante kwa kusaidia kushiriki " Kichocheo"!

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Joy Kauffman, MPH
Joy ni mwanzilishi mwenye shauku wa FARM STEW.
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.