Ilichapishwa
7 Novemba, 2019

Bustani: Uhuru kutokana na Njaa 

Robert Lubega

Uganda inajulikana kama "Lulu ya Afrika!" Ukiangalia, uzuri katika nchi na watu wake unang'aa kila mahali. Lakini wakaazi wengi wa vijijini wanaonekana kuwa hawana uwezo wa kuvunja ganda ili kupata lulu.

Moja ya vikwazo muhimu zaidi ni mtazamo wao. Hawana matumaini na wanakukosa motisha.

"Kabla ya kuja , fedha kidogo amabzo mume wangu angeweza kupata kama mshonaji wa viatu  hazikuwa zikitosha kulisha familia na kulipa karo ya shule kwa watoto wetu wanane.  Mimi niliogopa kulima (kilimo) kwani nilifikiri ni laana, "alisema Fatuma (katikati hapa chini).

Zawadi zako husaidia kubadilisha akili na mioyo ya watu waliopewa mafunzo na  FARM STEW.

Robert, mtaalamu wa kilimo wa FARM STEW, (kwa kijani), alitumia muda na David, na mkewe Fatuma hivi karibuni wakati wa moja ya ziara nyingi za nyumbani za FARMSTEW. Kwa kweli alivutiwa na bustani yao mpya inayostawi.  David, Fatuma na familia zingine nyingi zilionyesha matokeo ya mbinu walizojifunza kutoka kwa FARM STEW.  Hapa kuna vile Fatuma alivyoshiriki:

"Baada ya FARMSTEW kutufundisha faida ya bustani na kutupatia mbegu za mboga, ilifanya hatua yangu ya mageuzo.  Sasa ninajiona kama mtu muhimu sana katika jamii yangu. Kwa kulima mboga, tunaweza kumudu kuwatayarisha kula na tuna afya bora zaidi.
Baadhi ya wananchi katika jamii sasa wanakuja kununua mboga za majani. Sasa nina mboga katika hatua zote za ukuaji;zilizo bado katika shamba la miche zilizokua na zile zilizo tayari kuvunwa. Kwa kuuza zile za ziada, sasa ninaweza kuwapeleka watoto wangu shule na kutimiza mahitaji ya msingi ya nyumbani. Ninamsaidia hata mume wangu."


Wanandoa hawa wenye furaha wananikumbusha ukweli rahisi: FARMSTEW ni kazi nzuri ya umisionari! Nukuu hii iliongoza kazi ya FARM STEW:

Wakati mbinu sahihi za kilimo zinatekelezwa, umasikini utapungua zaidi kuliko ulivyo sasa. Tuna nia ya kuwapa watu mafunzo ya uzoefu kuhusu kuboresha ardhi, na hivyo kusababisha ari kulima nchi yao  ambayo haina kilimo kwa  sasa. Kama tutakamilisha hili, tutakuwa tumefanya kazi nzuri ya utume. — Ellen G. White, barua 42, 1895

Fatuma hayuko peke yake, kutokana na mafunzo ya FARM STEW maelfu ya maisha ya watu na ardhi imebadilishwa.

Bwana Bogere hakujua jinsi ya kulima bustani. Sasa anafundisha kijiji chake chote!
Mafunzo ya FARMSTEW yanawasaidia watu kama Mheshimiwa Bogere kubadilisha ardhi isiyotumika kuwa ya kilimo cha uzalishaji !

Asanteni kwa kufanya kazi hii iwezekane ili wenyeji wa Afrika waweze kupata baraka katika udongo!

Shiriki
Shiriki
Iliyotumwa na 
Robert Lubega
Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.

Kisa cha Naki
Uganda, Afrika
Manukuu
"Nina umri wa miaka kumi na minne (14) na nilianza hedhi mwaka huu. Siku yangu ya kwanza nilihisi aibu na nikakosa kwenda shule ... Si rahisi kupata visodo katika kijiji changu na vichache vilivyoko ni bei ghali. Visodo hivi vipya vitaweza kunisaidia nikiwa katika hedhi. Kwasababu vinaweza kutumika tena, sitakuwa na wasiwasi tena nitakapopata hedhi!"
Visodo

Uhuru kutokana na aibu

Kila siku maelfu ya wasichana wa Kiafrika huacha shule. KWA NINI?  Kwa sababu ya hedhi . Unaweza kuwasaidia wasichana hawa kuendelea na masomo yao  shuleni kwa  kuwapa visodo vinavyoosheka, chupi na kuwapa ujasiri kwa  dola kumi na tano ($15 ) kwa kila msichana  
Lengo letu ni   kuwafikia wasichana  5000 katika mwaka wa 2020!

Irene
Uganda, Afrika
Manukuu
Maisha ya Irene yatabadilishwa wakati zawadi zako zitakapoleta maji safi kwa jamii yake
Ishara ya maelezo
Kila dola  mbili ($2 )zinazopewa FARM STEW zitazidishwa kwa dola moja ($1) na Water4, hadi  dola elfu themanini na nne ($84,000).
Maji

Uhuru kutokana na Ugonjwa na kazi ngumu

Watu elfu 300 hufa kila siku kutokana na magonjwa yanayosababishwa na maji machafu. Zawadi yako inaweza kutoa maji safi kwa dola kumi na tano ($15) kwa kila mtu.  Maji salama sio tu huimarisha afya; bali hutoa fursa kwa ajili ya FARM STEW, kwa ushirikiano na makanisa ya mtaa  kutosheleza kiu ya kiroho ya wale walio na mahitaji.