Mgogoro

Njaa, ugonjwa na umaskini husababisha mateso makubwa.

FARM STEW Uganda

Miradi yetu

Ili kufanikisha mabadiliko,tunaendelea kufanya kazi katika miradi ifuatayo.

Maji
Irene ni mmoja wapo wa watu  663,000,000 ambao hawana uwezo wa kupata maji safi. Pampu ya maji kijijini mwao ilivunjika miaka iliyopita, pamoja na asilimia  thelathini (30%) ya pampu zote barani Afrika. Sasa FARM STEW inatoa chanzo cha matumaini kwa hali ya maji ili kuzima kiu yao ya kimwili na kiroho ($15 kwa kila mtu).
Mabomba ya mifereji
Teknolojia rahisi kama vile bomba la mfereji, linaloweza kutoa maji yanayo tiririka, pamoja na sabuni au majivu, linaweza kusafisha mikono bila uharibifu mwingi. FARM STEW inahimiza mabomba ya mifereji kwenye nyumba zote!
Visodo vya kufulika kwa Wasichana
Ulimwenguni kote wanawake na wasichana wengi hawana uwezo wa kupata visodo i, vyoo safi binafsi, au njia safi za kujikimu wakati wa hedhi. Tunaleta  heshima kwa wasichana kwa kuwafundisha na kuwaandaa kwa kuwapa vifaa wanavyo hitaji.
Mashamba madogo ya familia 
Ili kuwezesha familia za mashambani kuwa na kujitegemea na kutoa fursa kwa biashara, tunasambaza mbegu za kuanzia na vifaa vinavyohitajika kuanzisha ukulima wa mashamba madogo. Wanafanya mengine yaliyo salia kwa msaada wa wakufunzi wetu wa FARM STEW!
Mafunzo
Wakufunzi wetu wa FARM STEW wanasisitiza kanuni za kila mojawapo ya viungo vyetu vinane katika madarasa tunayoyafunza. Shughuli za kiutendaji hufanya masomo  kuchangamsha na kuwasaidia washiriki kustawi!
Mgogoro wa

Njaa

Utapiamlo unaendelea kuongoza kama mzigo wa kimataifa wa ugonjwa.
Umechangia karibu nusu ya vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano – zaidi ya  Virusi Vya Ukimwi/ UKIMWI (VVU/UKIMWI), malaria na kifua kikuu pamoja.

Afrika Mashariki ni kanda katika ulimwengu unaoendelea yenye kiwango  cha juu zaidi cha udomavu, kwa asilimia thelathini na tano nukta sita (35.6), hali ya mtapiamlo wenye athari kubwa isioweza kubadilishwa.


Kwa kujibu, FARM STEW ilianza na mkakati rahisi wa kuwalisha watoto.

Mgogoro wa

Ugonjwa

Utapiamlo unawaweka watoto katika hatari kubwa ya kufariki kutokana na maambukizi ya magonjwa ya kawaida, huongeza mzunguko na ukali wa maambukizi hayo, na kuchelewesha kupona. Wanawake na watoto ni miongoni mwa idadi kubwa ya watu wenye hatari zaidi ya masuala haya ya utapiamlo. Mara nyingi husababisha vifo vya mapema. Watoto wa mashambani mara nyingi wana uwezo wa  asilimia arubaini na tano(45%) zaidi  ya uwezekano wa kifo.

Upungufu wa lishe huchangiwa na  mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na udongo  usio na rutuba, usafi wa mazingira na kiwango cha chini cha lishe bora. FARM STEW hushughulikia mambo haya yote kwa kuzingatia siku1,000 za kwanza za maisha.
 Sarah, mtoto mdogo hapo chini ana dalili za udumavu na ukosefu wa protini

Mgogoro wa

Umaskini

Wakati idadi ya jumla ya maskini duniani imepungua katika miongo ya hivi karibuni, asilimia ya wale wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara imeongezeka kutoka 17.4% hadi 27.7%.

Umaskini uliokithiri, unaopimwa kwa dola 1.90 kwa kila mtu kwa siku, huathiri sana watoto.
Milioni 387, au asilimia 19.5 ya watoto duniani, wanaishi katika umaskini uliokithiri!

"Kwa kadiri ulivyofanya kwa uchache wa haya, umenitendea"
Yesu katika Mathayo 25:40

Ndiyo maana tupo na tunajali.